• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

Zaidi ya Bilioni 10 zatekeleza miradi ya Kimaendeleo Tarafa ya Mawengi Wilayani Ludewa kwenye Elimu, Afya, Maji, Barabara na Mawasiliano

tarehe Iliyowekwa: September 4th, 2023

Na. Mwandishi wetu - Ludewa

Tarafa ya Mawengi Wilayani Ludewa imepata fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo inayotekelezwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Afisa wa Habari na Mawasiliano Serikalini Wilayani Ludewa Ndugu. Chrispin Kalinga amesema serikali inaendelea kutekeleza miradi katika nyanja zote za Elimu, Afya, Maji, Barabara pamoja na Minara ya Mawasiliano ya simu.

Amesema katika nyanja ya Elimu kata zote zipatikanazo Tarafa ya Mawengi zimepata miradi  kupitia vyanzo mbalimbali vya fedha ikiwa ni pamoja na fedha za Mapato ya ndani na Fedha za Mradi wa Boost ambazo zimewezesha kujenga madarasa kwa baadhi ya kata ikiwemo kata ya Ludewa  katika shule ya Msingi Ludewa Mjini ambayo  imepokea fedha ya ujenzi wa madarasa 2 na matundu 6 ya vyoo ambayo tayari yamekamilika.

Aidha, akaongeza kwa kusema kuwa, kata zingine zimepata miradi ya ujenzi wa Hostel, pamoja fedha za ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Mawengi.

"Binafsi ninakila sababu ya kumpongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutupatia fedha za kuteketeza Miradi hii mikubwa, lakini pia ninakila sababu ya kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Ludewa Mhe. Joseph Kamonga kwa kupaza sauti awapo bungeni na ndio maana leo miradi hii inaletwa kwenye Wilaya yetu" alisema Bw. Kalinga.

Akaongeza kwa kusema kuwa, akiwa Kama Afisa habari na Mawasiliano Serikalini ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa atahakikisha anaendelea kuipitia miradi yote na kuwahabarisha wananchi wote wa Wilaya ya Ludewa na watanzania wote kwa ujumla wake jinsi Ilani ya Uchaguzi ya chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020/2025 invyotekelezwa kwenye kila kada ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa.

Katika ziara yake iliyoanza Septemba 1 mwaka huu katika Tarafa ya Mawengi ametembelea miradi na kuhamasisha wananchi kufanya Utalii wa Ndani na kuvitangaza vivutio hivyo kwenye maeneo yao ambapo jana Septemba 03 amehitimisha ziara hiyo katika Tarafa ya Mawengi kwa kupanda Mlima Mrefu nyanda za juu kusini Mlima unaojulikana kwa jina la Livingstone - Madunda akiwa na zaida Vijana pamoja wananchi 120.

"Leo tumefanikiwa kuupanda Mlima Mrefu wa Livingstone wenye historia nzuri na ya kipekee, niwaombe wananchi wote wa Ludewa kuanza kufanya Utalii wa Ndani ya Wilaya yetu kwani hakuna mtu anayeweza kuutangaza Utalii kutoka nje Kama sio sisi wenyewe tutasimama na kuvitembelea, Serikali tayari tumeanza kuyafikia Maeneo yote ya vivutio vya Utalii na kuyafikia Maeneo hayo na ndio maana leo tupo hapa". Alisema Chrispin Kalinga

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.