• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA LUDEWA AWAASA WATUMISHI WAPYA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO KUJIJENGA KIUCHUMI

tarehe Iliyowekwa: September 2nd, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Ndugu Sunday Deogratias, ametoa wito kwa watumishi wapya 43 kutoka kada za afya na kilimo walioripoti wilayani humo kuhakikisha wanaangalia maendeleo yao binafsi kwa kufanya kazi kwa bidii na kutumia fursa zilizopo katika maeneo yao ya kazi.


Akizungumza katika semina maalum ya kuwakaribisha watumishi hao wapya iliyofanyika leo katika ukumbi wa Halmashauri, Ndugu Deogratias amewataka watumishi hao kuwa na mtazamo chanya wa kujiletea maendeleo kupitia fursa nyingi zinazopatikana wilayani humo.


“Wilaya ya Ludewa imezungukwa na fursa nyingi. Ardhi bado ipo ya kutosha, bei za kununua au kukodi mashamba si kubwa kama ilivyo maeneo mengine. Halmashauri yetu ina kanda tatu zinazofaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali – hiyo ni fursa. Fikeni vituoni mkatafakari ni nini mnaweza kufanya zaidi ya kazi ya kila siku,” alisema Mkurugenzi.


Amewahimiza pia kutumia nafasi hiyo kujenga maisha yao mapema kwa kuwekeza katika miradi mbalimbali ya kiuchumi ikiwemo kilimo na ufugaji. “Napenda kuwaona mkijenga nyumba nzuri kabla ya kustaafu. Napenda watumishi ambao wamejijenga kiuchumi, manung’uniko hayatakuwepo,” alisisitiza.


Aidha, Mkurugenzi huyo amewakumbusha kuhusu miradi mikubwa ya kimkakati inayotarajiwa kuanza hivi karibuni katika wilaya hiyo, ikiwemo miradi ya Liganga na Mchuchuma, na kueleza kuwa uwekezaji huo utavutia watu wengi hivyo kuongeza mahitaji ya bidhaa na huduma mbalimbali.


“Watu wengi watakuja Ludewa, mahitaji yataongezeka. Hii ni fursa. Nawasihi mjihusishe na kilimo, ufugaji na shughuli nyingine zitakazowawezesha kuimarisha uchumi wenu binafsi. Mtumishi akiwa na uchumi mzuri hata malalamiko yanapungua,” aliongeza.


Watumishi hao wamepokea maelekezo hayo kwa mshikamano na kuahidi kujituma katika kazi na kuzingatia ushauri walioupata ili kuleta tija binafsi na kwa wananchi wa Ludewa kwa ujumla.

Matangazo

  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA RUZUKU YA MIRADI YA MAENDELEO 2025/2026 September 09, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA LUDEWA AWAASA WATUMISHI WAPYA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO KUJIJENGA KIUCHUMI

    September 02, 2025
  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.