• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

WATENDAJI WA KATA WAKABIDHIWA PIKIPIKI LUDEWA

tarehe Iliyowekwa: February 24th, 2023

Maafisa watendaji wa kata 8 za Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa wamekabidhiwa pikipiki zilizotolewa na serikali kwa lengo la kuboresha utendaji kazi na kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi hapa nchini.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi pikipiki hizo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Mhe. Wise Mgina, amesema kuwa pikipiki hizo ni vifaa muhimu kwa Maafisa hao zinazokwenda kumaliza changamoto ya kutembea umbali mrefu kuwafikia wanachi ili kutoa huduma.

Ameweka wazi kuwa, kata hizo 8 ziko maeneo ya pembezoni zikiwa na maeneo makubwa ya kiutendaji hivyo Maafisa hulazimika kutembea muda mrefu kuwafikia wananchi kutoa huduma jambo ambalo linakwenda kumalizika sasa.

Aidha amewataka Maafisa hao kutumia pikipiki hizo kwa ajili ya kazi iliyokusudiwa na serikali ya kuwahudumia wananchi na si vinginevyo huku akiwasisitiza kuzitunza na kuzithamini kwa kutambua kuwa ni mali ya Umma.

"Tunamshukuru Mhe. Rais kwa kuwathamini Maafisa Watendaji wa kata, kwa kuwa wao ndio wanawahudumia wananchi moja kwa moja, Watendaji mnalo deni sasa, mkatumie vifaa hivi kulingana na malengo yaliyokusudiwa na si kwa matumizi binafsi". Amesisitiza Mwenyekiti Wise Mgina.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Ludewa, Komredi Stanley Kolimba, ameipongeza serikali kwa kuteketeleza Ilani ya Chama hicho kwa vitendo, kwa kuhakikisha watumishi wanapata vitendea kazi vitakavyorahisisha utoaji na upatikanaji wa huduma kwa wananchi katika maeneo yao.

"Serikali inawategemea, mmepata usafiri, tumieni muda mwingi kutatua kero na changamoto za wananchi kwenye maeneo ya vijiji na vitongoji vyenu kwa wakati, kwa kufanya hivyo, tutafikia malengo ya serikali ambayo ndio maagizo ya Ilani".  Mwenyekiti CCM Kolimba

Zoezi hilo la kuwakabidhi pikipiki limeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Mhe. Victoria Mwanziva katika viwanja vya ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa.

Kwa upande wao Maafisa Watendaji kata, wameipongeza serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kuwapatia usafiri, jambo ambalo wamekiri lilikiwa ni changamoto kubwa iliyokwamisha utendaji kazi katika maeneo yao.

"Kupitia pikipiki hizi zinakwenda kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wetu, jambo la kufanya siku nzima sasa tutatumia saa moja, tunamshukuru Mama Samia na tunaahidi kuwahudumia wananchi kwa kasi kubwa sasa". amefafanua Maria Ngatunga Mtendaji wa Kata ya Madope.

Halmashauri ya wilaya ya Ludewa ni miongoni mwa Halmashauri nchini iliyopata pikipiki 8 kati ya pikipiki 916 zilizotolewa na serikali na kuzigawa kwa Maafisa Watendaji wa  kata.

#Ludewa ya Utalii, Uchumi wa Chuma na Mkaa ya Mawe kwa Maendeleo Yetu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.