• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

WATALII WAENDELEA KUMIMINIKA TANZANIA

tarehe Iliyowekwa: September 26th, 2022

Waziri wa maliasili na utalii Mhe. Pindi Chana,amesema kwa kipindi cha mwezi januari hadi julai mwaka huu jumla ya watalii zaidi ya 4000 walikuja nchini ikilinganishwa na watalii kwa kipindi cha januari hadi julai 2021.

Hatua hiyo imeelezwa  jana na waziri huyo wakati wa uzinduzi wa mkakati wa kutangaza utalii kusini mwa Tanzania uliofanyika mkoani Njombe ambapo alisema ni mafanikio ya mpango wa Royar Tour na kwamba watalii wanaendelea kumiminika.

Akizungumzia changamoto alisema licha ya sekta ya utalii kuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa nchi lakini mchango huo hauakisi utajiri wa rasilimali za utalii zilizopo hapa nchini.

Pindi alisema changamoto nyingine inatokana na watalii wengi wanaokuja nchini kutembelea zaidi vivutio vya utalii vilivyopo ukanda wa kaskazini ikiwemo hifadhi za taifa za Kilimanjaro, Serengeti, Ziwa Manyara na eneo la hifadhi ya Ngorongoro.

Alisema hali hiyo inasababisha siku za watalii  ambao wanakuja hapa nchini kukaa kuendelea kuwa chache na watalii kutojirudia.

Alisema katika kufungua utalii kwenye vivutio vya nchi mwaka 2017 serikali ilianzisha mradi wa kuboresha usimamizi wa maliasili na kukuza utalii kusini mwa Tanzania kwa lengo la kupanua wigo wa mazao ya utalii kijiografia kwa kuendeleza sekta hiyo katika mikoa ya kusini.

"Mradi huo unatekelezwa kupitia fedha za mkopo wa masharti nafuu wa dola za Marekani milioni 150 kutoka benki ya dunia" alisema Dk. Chana.

Alisema katika kufanikisha azma ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo mikoa ya kusini wizara ya maliasili na utalii kupitia bodi ya utalii Tanzania imeendaa mikakati mahususi ya kutangaza vivutio vya utalii.

Kaimu mkurugenzi wa bodi ya utalii Tanzania Felix John,alisema utalii ni moja ya sekta za vipaumbele hapa nchini na Rais Samia Suluhu Hassan amejitoa kupitia programu maalum ya Tanzania Royal Tour ili kuitangaza na kuifungua nchi katika sekta ya utalii.

John alisema bodi hiyo imejipanga ili kufungua utalii wa nyanda za juu kusini kwa kuleta watalii kwenye vivutio vilivyopo katika mikoa hiyo.

"Kama mnavyofahamu vipo vivutio vingi katika ukanda huu wa kusini tunayo Kitulo, Mpanga Kipengele na eneo la kihistoria la nyumbanitu" alisema John.

Mkuu wa mkoa wa Njombe Anthony Mtaka alisema Tanzania ina hifadhi nyingi na zinafanana lakini upekee uliopo kwa mkoa wa Njombe ni hifadhi ya Kitulo ambayo ni maalum kwa uhifadhi wa maua.

"Kwa maana kama shughuli inafanyika Dar es salaam haya maua inabidi waagize kutoka sehemu nyingine lakini kama ni Njombe yanapatikana hapa hapa" alisema Mtaka.

Alisema watu wengi hawafahamu kuwa hata biashara ya maua inayofanyika mkoa wa Kilimanjaro wilaya ya Moshi na Arusha ilianzia mkoani Njombe.

Alisema biashara hiyo haikufanyika mkoani Njombe kutokana na kukosekana kwa miundo mbinu ya  uwanja wa ndege.

Baadhi ya wabunge wa mkoa wa Njombe wakiwemo Joseph Kamonga na Deo Sanga walisema ili utalii ulete tija kwenye mkoa wa Njombe waliiomba serikali kuharakisha ujenzi wa uwanja wa ndege kwasababu utalii unakwenda sambamba na usafiri wa uhakika.

"Uwanja wetu wa ndege hapa ukamilike ili watalii wawe wanashuka na kuja kwa njia ya ndege na mambo mengine kama kusafirisha parachichi zetu" alisema Sanga.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.