• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

WANAFUNZI LUDEWA WAPEWA ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA DAWA ZA BINADAMU

tarehe Iliyowekwa: October 18th, 2023

Na. Chrispin Kalinga - Ludewa

Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imetoa elimu ya matumizi sahihi ya dawa, vifaa tiba pamoja na vitendanishi  kwa makundi mbalimbali ya kijamii na wanafunzi wa Wilaya ya Ludewa  ili kuzuia madhara yanayoweza kutokea kutokana na utumiaji wa dawa  kiholela.

zoezi hilo limefanyoka leo Oktoba 17, 2023 katika shule ya Sekondari St. Alois iliyopo Wilayani Ludewa na  wananchi waliofika kupata huduma za kiafya katika hospitali ya Wilaya ya Ludewa.

Akizungumza  na wanafunzi wa shule hiyo  mkaguzi wa dawa BW. Adam Sarota  amesema mafunzo hayo yamelenga kutoa elimu pamoja na kujifunza kutoa taarifa ya madhara yanayotokana na matumizi ya bidhaa hizo.

Aidha, amesema matumizi yasiyo sahihi ya dawa na vifaa tiba na vitendanishi yanasababisha athari kubwa kwa watumiaji, watu kupoteza maisha, kupata ulemavu na viungo mbalimbali kuathirika kama ini na, figo.

Sarota  alisema utoaji wa elimu hiyo itakuwa endelevu ili wananchi waweze kujua namna bora ya matumizi ya dawa na ndio maana wameanzisha klabu za TMDA  katika shule za mkoa wa Njombe mbalimbali ili elimu hiyo inayotolewa na TMDA iweze kusambaa kila maeneo na kuifanya jamii kuelewa athari za matumizi ya dawa hizo.

Mkaguzi alitoa wito  kwa wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya dawa ikiwemo kuepuka matumizi holela ya dawa kwa kutumia dozi kikamilifu sambamba na kupata vipimo na ushauri wa wataalam wa Afya kabla ya kutumia dawa hizo.

"Kuna baadhi ya watu  katika jamii wanatumia dawa kiholela na sisi TMDA tunaendelea kuwaelimisha kuwa utumiaji wa dawa kiholela unaweza kusababisha usugu wa vimelea na kufanya dawa hizo kushindwa kufanyakazi kama inavyotakiwa" alisema Sarota

Aidha aliwataka wanafunzi hao kufikisha elimu hiyo kwa wazazi na walezi na jamii kwa ujumla kwa lengo la kuendelea kulinda afya ya jamii

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.