• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

WADAU WA LISHE LUDEWA WAKUTANA KUJADILI CHANGAMOTO ZA LISHE NA UTATUZI WAKE

tarehe Iliyowekwa: March 4th, 2021

Wadau wa Lishe Wilayani Ludewa wamekutana katika kikao cha dharula ili kutathmini hali ya Lishe katika Wilaya hiyo. Mratibu wa Lishe Wilayani humo Bi. Neema Noah amesema wamelazimika kukutana kwa dharula licha ya kwamba hivi karibuni walikuwa wamekaa katika kikao cha kawaida cha tathmini ya robo mwaka katika robo ya pili. Kikao hicho kiliongozwa na Bi. Gladness Mwano ambaye ni Afisa Utumishi na Utawala wa Wilaya akimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo. akizungumza katika Kikao hicho Bi Mwano amesema kwamba anawashukuru wajumbe wote walioshiriki kikao hicho muhimu kwani ni kwa maendelea ya afya ya Wanaludewa kwa ujumla, hususani katika kuangazia tatizo sugu la udumavu ambalo limekuwa likilalamikiwa na wadau wengi wa maendeleo Wilayani humo ukizingatia ni Wilaya yenye upatikanaji mkubwa wa Chakula katika Mikoa ya Nyanda za juu kusini.

Kikao hicho ambacho pia kimehudhuriwa na Viongozi wengi sana wa Dini na madhehebu kimekuwa chenye ufanisi kwani mchango mkubwa ulitolewa na Wajumbe, hasa viongozi wa Dini ambapo kwa mtazamo wa Wataalam wa Halmashauri walioshiriki kikao hicho, imeleta hamasa sana kwa maana kwamba ujumbe utafika kwa watu wengi zaidi kwa wakati mmoja na muafaka ikizingatiwa viongozi wa Dini wanajukwaa kubwa la kukutana na wananchi. Viongozi wa Dini walioshiriki kikao hicho ni kutoka Kanisa Katoliki,Bakwata, Sheikh wa Wilaya ya Ludewa, Anglikana,KKKT, TAG, EAGT pamoja na Watendaji wa Kata na wadau wa Lishe. Maeneo kadha yaliyoangaziwa katika kikao hicho ni pamoja na hali ya lishe katika mkoa kwa watoto chini ya miaka mitano, utapiamlo na aina za utapiamlo, mathalani udumavu, ukondefu, uzito pungufu na ukosefu wa vitamini na madini mwilini. Pia kikao hiki kiliangazia sababu za udumavu, athari za udumavu kwa watoto na jamii kwa ujumla, haki za mtoto ikiwemo haki ya kuishi, kuendelezwa, kulindwa, haki ya kushirikiswa katika masuala yanayowahusu watoto wenyewe na haki ya kutobaguliwa. Halikadhalika wajumbe wa kikao waliangazia maeneo yanayopaswa kutekelezwa kama wajibu wa wadau mbalimbali katika jamii katika makundi mbalimbali kama vile wajibu wa wazazi katika malezi, wajibu wa viongozi wa dini katika jamii na wajibu wa jamii nzima kwa ujumla ili kukabiliana na changamoto za lishe kwa watoto katika umri wa kuanzia ujauzito, kuzaliwa mpaka angalau miaka 2 toka kuzaliwa, ambayo kitaalamu imeelezwa kwamba ni siku elfu moja (1000) za kukabiliana na lishe duni kwa watoto. Akihitimisha kikao hicho, Mwenyekiti wa kikao na Afisa Utumishi wa Wilaya hiyo Bi. Gladness Mwano amewashukuru wajumbe wote na kuwaasa kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake kwa jamii, hususani kundi lengwa la watoto wadogo ili kuikoa jamii na madhara yatokanayo na lishe duni katika Wilaya yetu

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.