• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

SHIRIKIANENI KUWALINDA WATOTO

tarehe Iliyowekwa: June 3rd, 2022

Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wazazi na walezi washirikiane na walimu katika kuwalinda watoto wa kike na wa kiume ili waweze kutimiza ndoto zao kielimu.

Pia, Waziri Mkuu amewataka watoto hao wasikubali kudanganywa na watu wasiopenda maendeleo yao na badala yake wasome kwa bidii na wahakikishe malengo yao kielimu yanatimia.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Juni 3, 2022) alipozungumza na wanafunzi, wazazi na walimu katika shule ya Sekondari Mandarawe wilayani Ruangwa akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humo.

“Kwa sasa kielimu wilaya yetu imepiga hatua kubwa, wanafunzi someni  kwa bidii na Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha kwamba inawawezesha  kutimiza malengo mliyojiwekea.”

Mheshimiwa Majaliwa amesema Kata zote za Wilaya hiyo zina shule za sekondari na tayari wameanza ujenzi wa mabweni, lengo likiwa ni kuwapunguzia wanafunzi adha ya umbali mrefu kwenda shuleni.

“Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa kila mtoto wa Kitanzania aliyefikia umri wa kwenda shule apelekwe shule na elimumsingi inatolewa bila ada nchini kote.”

“Kwenye suala la elimu tumejipanga vizuri na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ametuunga mkono kwa kutupa sh. milioni 700 za ujenzi wa shule ya sekondari wasichana ya mchepuo wa Sayansi.”

Pia, Waziri Mkuu amekagua ujenzi wa Kituo cha Afya cha Namichiga na ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wananchi wasimamie vizuri mradi huo na wahakikishe fedha zinatumika vizuri.

Mbali na kukagua ujenzi wa kituo hicho, pia Waziri Mkuu alikagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo vya Afya cha Kata ya Narungombe pamoja na maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya cha Nangurugai.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Majaliwa amewasisitiza wananchi wahakikishe wanatunza mazingira na kuacha kukata miti hovyo. “Tutunze  mazingira na tusilime katika vyanzo vya maji.”

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.