• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

MRADI NA. 5441-TCRP, MKURUGENZI AKABIDHI VYUMBA VYA MADARASA CHIEF KIDULILE

tarehe Iliyowekwa: December 23rd, 2021

MRADI NA. 5441-TCRP, MKURUGENZI AKABIDHI VYUMBA VYA MADARASA CHIEF KIDULILE SEKONDARI; UKAMILISHAJI MAENEO MENGINE UNAENDELEA KWA KASI

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Bwana Sunday Deogratias amemkabidhi Mheshimiwa Andrea Tsere, Mkuu wa Wilaya ya Ludewa vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Sekondari Chief Kidulile. Katika Hafla fupi iliyofanyika Shuleni hapo, Mkuu wa Wilaya ya Ludewa amemshukuru Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuipatia Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa fedha kiasi cha Tsh. 940,000,000/= (Mia Tisa Arobaini Milioni) ambazo zimewezesha ujenzi wa Vyumba vya madarasa 47 katika Shule zote 17 za Sekondari zilizipo katika Halmashauri hiyo.

Katika Picha, Mheshimiwa Andrea Tsere (watatu kutoka kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Ludewa akiwa katika picha ya Pamoja na Mheshimiwa Monica Mchilo (kulia kwake) na Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Sunday Deogratias na wajumbe wa kamati ya Ujenzi ya Chief Kidulile baada ya makabidhiano ya vyumba vinne vya madarasa.

Aidha amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha anawasimamia watendaji na uongozi katika Shule hiyo kuhakikisha wanalinda miundombinu yote ya mradi huu kwani Serikali Inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haitakubali kuona mradi unaharibiwa mapema kabla hata ya kupata matokeo yaliyokusudiwa. Amemtaka kumuagiza Mkuu wa Shule hiyo kuweka alama maalumu katika viti na meza za wanafunzi kabla ya kuwagawia, na wahakikishe wanawapa elimu ya kutunza samani hizo na majengo.

Katika habari picha ni viti na meza vikiwa vimepangwa katika moja ya vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Sekondari Chief Kidulile.

Katika hatua nyingine, Diwani wa Kata ya Ludewa Bi. Monica Mchilo ameishukuru Serikali inayoongozwa na Chama cha Mapinduzi, chini ya Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Kata yake ya Ludewa katika Shule hiyo Kiasi cha Tsh. Milioni themanini (80,000,000/=) zilizowezesha kukamilisha ujenzi wa madarasa manne, na hiyo itapelekea kuepusha msongamano wa wanafunzi pindi shule zitakapofunguliwa. Amemhakikishia Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Ludewa kwamba yeye na wananchi waliomchagua wa Kata ya Ludewa wanamuunga Mkono Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan katika juhudi kubwa anazofanya kuliletea maendeleo Taifa, ikiwemo Wilaya ya Ludewa ambayo imepatiwa fedha nyingi sana katika miradi mbalimbali.

Naye Mkurugenzi Mtendaji akitoa salam za shukrani kwa niaba ya uongozi na watendaji wa Halmashauri, Amemshukuru sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa fedha alizoipatia Halmashauri ya Ludewa katika Mradi huu (Mradi Na. 5441- TCRP), katika sekta ya Afya, Elimu, na amemhakikishia Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kwamba maagizo yote aliyoyatoa yatazingatiwa na kwamba atahimiza juhudi kubwa ziendelee katika kukamilisha mradi huu katika maeneo mengine, hususani Kata ya Makonde katika Sekondari ya Makonde kwani inakabiliwa na changamoto kubwa ya usafirishaji vifaa kupitia Ziwa Nyasa. Hata hivyo ameendelea kuwatia moyo wakazi wa Kata ya Makonde kwani licha ya changamoto hiyo, wamefikia hatua nzuri sana na atahakikisha anawasimamia wakamilishe kwa wakati ujenzi wa madarasa katika Shule iliyopo katika kata hiyo.

Sehemu ya ndani ya moja ya madarasa ya Shule ya Sekondari Chief Kidulile, katika Mradi Na. 5441-TCRP. Taa zikiwa zinawaka na viti na meza vimepangwa kwa unadhifu mkubwa, ikiwa ni ishara ya kukamilika kwa mradi katika Shule hii. Kazi Iendeleee.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Ndugu Sunday Deogratias, akitoa salam za Shukrani mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Ludewa (aliyeketi mbele kabisa kushoto) katika hafla ya makabidhiano ya vyumba vinne vya madarasa Shuleni Chief Kidulile Sekondari.


Diwani wa Kata ya Ludewa (CCM) Bi. Monica Mchilo akiteta jambo na Mheshimiwa Andrea Tsere, Mkuu wa Wilaya ya Ludewa katika hafla ya makabidhiano ya vyumba vinne vya madarasa ya Mradi Na.5441-TCRP. Wengine katika msitari wa mbele ni Ndugu Sunday Deogratias, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa (watatu kutoka kushoto) na Ndugu Onesmo V. Haule, Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Chief Kidulile.

Vyumba vinne vya madarasa katika Mradi Na.5441-TCRP katika Shule ya Sekondari Chief Kidulile baada ya kukamilika ujenzi wake na kukabidhiwa  kupitia Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Ludewa.

Madarasa ya Mradi Na.5441-TCRP muonekano wa upande wa nyuma baada ya kukamilika katika Shule ya Sekondari Chief Kidulile tarehe 23-12-2021.

Kwanza tupambe, kishaaaa tusherehekeeeee. Ndicho unachoweza kusema, baada ya Shughuli pevu, wananchi wa kata ya Ludewa, wakiongozwa na Mheshimiwa Monica Mchilo Diwani wao, wanafurahia kukamilika kwa Mradi Na.5441-TCRP, vyumba vinne vya madarasa vilivyogharimu Tsh. 80,000,000/= zilizotolewa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Shule ya Sekondari Chief Kidulile iliyopo katika kata ya Ludewa. Katika habari picha, Mheshimiwa Andrea Tsere na wadau mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya makabidhiano.

Ni furaha na vicheko tu baada ya kumalisha ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Sekondari Chief Kidulile.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.