• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

Mkurugenzi Mtendaji Ludewa ashiriki kikao Njombe

tarehe Iliyowekwa: November 25th, 2022

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Ndg.Sunday Deogratias leo Novemba 25 ameshiriki kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Njombe (RCC).

Pamoja na mambo mengine zimewasirishwa taarifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na taarifa ya elimu ambapo Afisa  elimu mkoa wa Njombe Nelasi Mulungu amesema kuwa


Jumla ya wanafunzi 963 wa shule za sekondari mkoa wa Njombe kati yao wavulana 584 na wasichana 379 sawa na asilimia sita hawakufanya mitihani yao ya kidato cha pili kutokana na sababu mbalimbali.


Akizungumza katika kikao cha kamati ya ushauri mkoa RCC, Afisa elimu mkoa wa Njombe Nelasi Mulungu alisema wanafunzi hao walianza kidato cha kwanza vizuri lakini walivyoingia kidato cha pili wakawa wamepotea.


"Wanafunzi waliofanya mtihani 2022 waliandikishwa shule ya sekondari mwaka 2021,kidato cha kwanza wakiwa jumla ya wanafunzi 15,256 kati yao wavulana 6,664 na wasichana 8,546 hivyo walistahili kufanya mtihani wa kidato cha pili mwaka 2022"alisema Mulungu.


Mulungu alisema watoto wengi watoro ni wavulana ambao inadaiwa kuwa wanakwenda kufanya vibarua mikoa ya jirani.


"Tumewajulisha mamlaka za halmashauri na wakuu wa wilaya kuwatafuta ili kurudi shule, kwa sababu mh Rais ametoa ridhaa kwa watoto wote ambao wameacha shule kwa sababu mbalimbali warudi shuleni,awe wa sekondari awe wa shule za msingi kwa hiyo mamlaka husika zinaendelea kuwatafuta"alisema Mulungu.


Ofisa ustawi wa jamii mkoa wa Njombe Subilaga Mwaigwisya,alisema changamoto kubwa inasababishwa na wazazi kuwaachia majukumu ya familia watoto wa kiume.


"Tumekua na ugomvi mkubwa na familia wazazi hasa kwa watoto wa kiume,baada ya baba labda kuondoka alafu yule mtoto wa kiume anachukua majukumu kama baba au wakati mwingine anaenda kufanya shughuli za kiuchumi zinaweza zikawa ni zake au za familia nzima kwa hiyo wengi wao wanaenda kujihusisha na shughuli za kiuchumi,kwenye kubeba mbao,biashara ndogondogo"alisema Mwaigwisya.


Hata hivyo alisema"Lakini kwa watoto wa kike ukiangalia hiyo takwimu tunao watoro lakini tunashindwa kujua wapo wapi kwa sababu hatuna ndoa za utotoni wala watoto wa kike wanaofanyishwa kazi kwa sababu tunafanya ukaguzi hata nyumba kwa nyuma ili mtoto wa kike aweze kupata elimu"alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.