• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango amezisisitiza Wizara kusimamia sheria.

tarehe Iliyowekwa: July 20th, 2023

Na Chrispin Kalinga

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango amezisisitiza Wizara kusimamia sheria na kutekeleza miradi iliyopo kwenye bajeti ya mwaka mpya wa fedha 2023/2024, na kuhakikisha fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya Makambako hadi Songea zinapatikana na matengenezo yanafanyika.

Mhe. Dkt. Mpango amesisitiza hayo leo aliposimama kuwasalimia wananchi wa Mkoa wa Njombe,eneo la tanki la maji katika Halmashauri ya Mji Makambako akielekea Songea mkoani Ruvuma.

Amesema kuwa,ipo haja kwa Wizara ya kilimo kusimamia sheria ili kutokomeza rumbesa,uuzaji wa mazao shambani na walanguzi wa mbolea ili mkulima anufaike kupitia kilimo na kufaidi jasho lake,kwa kuhakikisha mazao yote ikiwa ni pamoja na viazi vinapimwa kwa vipimo sahihi,walanguzi wa mbolea wanakoma kwa kuwachukulia hatua za kisheria bila kuwachekea.


Pia,amewataka wakulima wa zao la parachichi Mkoa wa Njombe kutouza parachichi ambazo hazijakomaa,kwa kushawishiwa na wanunuzi wenye nia ovu ili kuharibu sifa za bidhaa zinazozalishwa nchini ,na kuitaka Wizara ya kilimo kuendelea kutoa elimu kwa wakulima wa zao hilo juu ya athari za uuzaji wa  parachichi ambazo hazijakomaa.

Aidha,ameitaka Wizara ya fedha ,kutafuta fedha kwa ajili ya matengenezo  ya barabara ya Makambako hadi Songea,kwani barabara hiyo ni kubwa na inatumika kusafirisha mazao ya chakula na bidhaa nyingi kwa ajili ya Uchumi wa Mikoa hiyo na taifa kwa ujumla.

Lakini pia,ametoa wito kwa kina mama kuacha urembo wakunyonyesha kwa kuhakikisha wanakula vyakula vyenye virutubisho kipindi chote cha ujauzito hadi kujifungua,na kunyonyesha watoto kwa muda wa miaka miwili na kuhakikisha watoto wanakula vyakula vyenye virutubisho muhimu kwa afya zao, ili wapate lishe bora na kuwa na afya bora katika ukuaji wao.

Aidha,ametoa rai kwa wazazi kuwasomesha watoto wao kwani ni uwekezaji wa uhakika ,kwa manufaa yao na watoto wao,pamoja na kuchukua tahadhali juu ya maambukizi ya UKIMWI ili kudhibiti maambukizi mapya.
Viongozi mbalimbali kutoka Mkoa wa Njombe wakiwemo viongozi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa wameshiriki mkutano wa Mhe. Dkt. Mpango

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.