• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

MBUNGE MHE. DEO NGALAWA AWAASA WANA LUDEWA KUMUUNGA MKONO RAIS DKT. MAGUFULI

tarehe Iliyowekwa: August 17th, 2019

Mbunge wa Jimbo la Ludewa Mkoani Njombe Mhe. Deo Ngalawa amewaasa wananchi wa Jimbo la Ludewa Kumuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika juhudi kubwa anazofanya kuliletea Taifa letu Maendeleo. 

Akizungumza kwa hisia katika Kikao cha Baraza la Madiwani, Mhe. Ngalawa amesema Nchi hii ilikuwa imefika mahali pabaya sana kiasi kwamba maskini na wanyonge walikuwa hawana haki katika Taifa hili. Hivyo wakati Mheshimiwa Rais akifanya juhudi za makusudi kuleta usawa baina ya wananchi yapaswa kumuunga mkono juhudi zake kwa gharama zote na kwa moyo wote.

"Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais wetu amedhibiti mianya yote ya Rushwa, amekomesha ufisadi, matokeo yake sasa tunaona miradi mikubwa mingi ikitekelezwa kwa fedha zetu wenyewe" alisema Mheshimiwa Ngalawa. Aliongeza kwa kusema, sasa hivi Mhe. Rais amenunua Ndege nane kwa mpigo, ambapo sita tayari zimewasili nchini, anajenga Reli ya Standard Gauge, anajenga mradi mkubwa wa Umeme Mto Rufiji, Vituo vya Afya, hapa kwetu ametupatia fedha za kujenga na kukarabati vituo vinne na karibia kila kata nchini ujenzi wa vituo vya Afya, maboma ya shule unaendela na pia umekamilika maeneo mengi sana, Hospitali za Wilaya. Ni lazima tujivunie na Tumpongeze Rais wetu kwa juhudi hizi. 

Katika Mkutano huo wa Baraza la Madiwani uliofanyika siku ya Jumamosi tarehe 17, Agost 2019 Mheshimiwa Mbunge Ngalawa pia alishauri wananchi kuongeza juhudi katika mapambano dhidi ya rushwa, kukemea ufisadi na kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo. Alitumia Mkutano huu kumshukuru Mhe. Rais kwa Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha zege toka Iton-Ludewa-Manda kipande cha urefu wa kilometa 50 toka Lusitu mpaka Mawengi. Akizungumzia Mradi huu, Mheshimiwa Mbunge Ngalawa amesema kwa Wanaludewa, hii ni heshima kubwa sana kwetu kwani Ujenzi wa aina hii ni wa gharama kubwa sana, na urefu wa km 50 kwa kiwango cha zege ni wa kipekee katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Mh. Andrea Tsere amempongeza Mheshimiwa Mbunge Ngalawa kwa kushiriki Mkutano huo wa Baraza la Madiwani. Akitoa salaam za Serikali Kuu, Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema kwamba umoja na mshikamano ndio nguzo ya mafanikio ya Ludewa. Alisisitiza kwamba umoja na mshikamano uliopo kati ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Ofisi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Halmashauri yaani Mhe. Mwenyekiti, Madiwani wote, Wataalam na watumishi wote (Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji) wanafanya kazi kwa ushirikiano wa hali ya juu sana na hivyo kuleta tija kwa wananchi wa Ludewa na Taifa kwa ujumla. 

Amewataka wananchi wote kuhakikisha wanashiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.