• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

Mbunge Ludewa afanya Ziara ya kikazi kukagua Miradi

tarehe Iliyowekwa: May 30th, 2022

Mbunge wa Jimbo la Ludewa *Mhe. Joseph Kamonga* alifanya ziara kwenye baadhi ya miradi inayoendelea kutekelezwa ndani ya wilaya ya Ludewa, na kuweza kujionea maendeleo  ya miradi hiyo na changamoto wanazo kumbana nazo wakati wa utekelezaji.

Ziara ya Mheshimiwa Mbunge ilihusisha miradi ifuatayo.

*1. Shule ya Sekondari kata ya Lubonde.*
- Utekelezaji wa mradi huu kamati ilipokea kiasi Cha Tsh. 470,000,000 ambazo niza awamu ya kwanza na majengo yanayo takiwa kukamilika kwa fedha hiyo ni,

-Jengo la Utawala ambalo limefika hatua ya kuweka bimu.

- Madarasa nane yapo hatua ya kuweka bimu.

- Maabara 1 ipo hatua ya kuweka bimu.

- Maktaba ipo hatua ya kuweka bimu

- Vyoo vipo hatua ya kusimamisha ukuta

- Maabara mbili zipo hatua ya jamvi.

Licha ya changamoto ndogondogo zinazo wakumba lakin ujenzi unaendelea vizuri na wanachi wanajitoa kwa moyo kuhakikisha ujenzi unakamilika halaka na wanafunzi waanze kusoma.

*2. Shule ya Msingi Kiyombo.* 

Ujenzi wa vyumba viwili vya Madarasa na Nyumba pacha ( Nyumba yenye uwezo wa kuchukua familia mbili ) kwaajili ya walimu.

Utekelezaji wa mradi huu upo chini ya mfuko wa TASAF na unagharimu zaidi ya kiasi cha Shilingi milioni 111.

Ujenzi uneendelea vizuri na wanatarajia kumaliza mapema ili vyumba vya madarasa na nyumba ya Mwalimu ikamilike na kuanza kutumika ili kuongeza ufanisi katika shughuli nzima ya utoaji Elimu kwa wanakiyombo.

*3. Ujenzi wa VETA Shaurimoyo.*

Utekelezaji wa mradi huu Serikali imetoa Bilioni 5 na milioni 400 kwaajili ya ukamilishaji wa mradi huu na chuo kianze kutoa hudumu kwa wananchi.

Utekelezaji wa mradi huu unaendelea ijapo kuwa wapo nyuma ya mda kutokana na changamoto mbalimbali zinazo wakabili kama upatikanaji wa umeme wa uhakika na mchanga mzuri unaofaa kwaajili ya utengenezaji wa tofali, kwani malighafi hiyo wanaisafirisha kutoka Mkiu na Makambako.

Mheshimiwa Mbunge kawaasa kuongeza juhudi na ufanisi ili kuhakikisha ujenzi unakamilika mapema iwezekanavyo kwani serikali imeshatoa fedha zote kilichobaki ni utekelezaji wao na kukamilisha ujenzi kwa mdaa walio wekekewa.

*4. Ujenzi wa kituo Cha afya Mundindi* 

Utekelezaji wa kituo Cha afya Mundindi Serikali imetoa kiasi Cha Shilingi Milioni 500 kupitia fedha za tozo.

Kutokana na Sensa iliyofanyika mwaka 2012 Tarafa ya Liganga ina jumla ya wananchi 40,000, Hivyo kukamilika kwa kituo hiki Cha afya ambacho kimepewa hadhi ya kituo cha afya cha tarafa kitahudumumia wananchi zaidi ya Elfu 40 ndani ya tarafa.

Maendeleo ya Mradi huu yapo hatua nzuri na Hivyo wananchi wategemee kuanza kupata huduma mapema iwezekanavyo
.
- Jengo la Utawala na OPD lipo hatua za mwisho wanamalizia kupaka rangi ya awam ya pili.

- Jengo la Maabara nalo lipo hatua za mwisho na baadhi ya Vyumba vimekwisha kamilika

- Kizimba cha kuchomea taka kimesha kamilika

- Kwasasa kazi inayoendelea ni kuset msingi wa jengo la huduma ya mama na mtoto na wanaendelea vizuri na tutegeme kuanza kupokea  huduma.

*5. Ukaguzi wa barabara ya Muholo - Lugarawa*

 Pia Mheshimiwa Mbunge alipata wasaa wa kutembelea ujenzi wa barabara ya Muholo mpaka Lugarawa ambayo inaendelea vizuri na inapitika vizuri Kwasasa.

Barabara hii ilikuwa ina umuhimu mkubwa Sana kwani ilikuwa inaunganisha kata nne za Luana, Ludende, Mkongobaki na Lugarawa, Hivyo kukamilika kwake kutarahisisha usafiri kwa wananchi wa maeneo hayo kwenda makao makuu ya wilaya.

*6. Ukaguzi wa barabara ya Mbwila - Lifuma.* 

Barabara hii inaunganisha kata ya Luana Tarafa ya Mawengi na kata ya Lifuma iliyopo Tarafa ya Mwambao.Hadi sasa barabara hiyo imetengewa Kiasi ch milioni 250 na barua ya kuomba fedha zaidi imeishawasilishwa serikalini.

Mpaka sasa Km 1.7 ya barabara hiyo imeshafunguka kuanzia kijiji cha Mbwila.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.