• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

Ujenzi wa Shule Maalumu Ludewa: DC Tsere kuongoza mchakato wa uzinduzi katika eneo la ujenzi huko Songambele

Saturday 5th, July 2025
@Wilaya ya Ludewa-Songambele

Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Mheshimiwa Andrea Axwesso Tsere kesho Jumamosi August 31, 2019 anatarajia kuongoza mamia ya wakazi wa 

Wilaya ya Ludewa katika uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa Shule maalumu ya vipaji katika Wilaya hiyo. Uzinduzi huo katika hatua za awali 

unatarajia kushuhudia shughuli za kusafisha eneo la ujenzi wa shule katika eneo la Songambele kata ya Ludewa. 

Akitangaza mchakato wa zoezi litakavyoendeshwa, Katibu Tawala wa Wilaya ya Ludewa Bi. Zaina M. Mlawa 

amewaasa wananchi kujitokeza kwa wingi ili kuunga mkono juhudi za kujiletea maendeleo sisi wenyewe kwa kufanikisha 

ujenzi wa Shule hiyo kwani itakuwa ni kwa faida ya Wana Ludewa wenyewe. Amewaasa wananchi wa Kata ya Ludewa kufika

katika eneo la ujenzi wakiwa na vifaa vya kufanyia usafi kama vile makwanja, mapanga na reki kwa ajili ya usafi huo kuanzia

majira ya saa mbili kamili asubuhi. Aidha amesisitiza wananchi wote kujitokeza kwa wingi kwani ni sehemu ya siku maalumu

ya usafi wa kila mwezi kama ilivyo utaratibu wa usafi kila mwisho wa mwezi. Katika mradi huo wa ujenzi wa Shule maalum

kulikuwa na zoezi la harambee ya kuchangia ujenzi ambapo mpaka sasa kiasi cha Tshs. milioni arobaini na moja  (Tsh.41m) zimepatikana.

Ambapo akitoa tathmini, Mkuu wa Wilaya amesema fedha hii inatosha kwa wastani kujenga vyumba viwili vya madarasa, hivyo wadau

zaidi wanaombwa kuendelea kuchangia ili kufanikisha azma hii. Zoezi hili ambalo mchakato wake ulianza mapema mwezi Februari, 2019

litakuwa endelevu na wadau wote walioshiriki na kutoa ahadi anawapongeza kwa ahadi zao ambazo zitasaidia kufanikisha lengo hili.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndg. Sunday Deogratius amewataka watumishi wote waliopo katika

kata ya Ludewa wakiongozwa na wakuu wao wa Idara na Vitengo kuhakikisha wanashiriki zoezi hilo ili kuwatia moyo

wananchi wao wanaowatumikia. Amesema ni ishara nzuri ya umoja, ushirikiano na mshikamano ambao watumishi

wa umma na wananchi wa Ludewa wamekuwa wakishikamana muda wote kwenye masuala ya msingi kama haya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.