• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

WAKALA WA MBOLEA AKAMATWA MJINI NJOMBE

tarehe Iliyowekwa: January 19th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthon Mtaka amefanya ziara ya kikazi leo katika   halmashauri ya Mji Njombe Kata ya Ramadhani mtaa wa Mgodechi,Kufuatia kukamatwa kwa shehena ya mifuko ya mbolea inayodaiwa kutumika kufanya uchakachuaji na udanganyifu leo hii, kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Njombe ikiongozwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Antony Mtaka wamefika kwa wakulima walionunua mbolea siku chache zilizopita na waliokiri kununua mbolea iliyofanyiwa udanganyifu kutoka kwa mfanyabiashara jina lake limehifadhiwa anayeshukiwa kukutwa na shehena hiyo ya mifuko inayokadiliwa kuwa zaidi ya 10,000.

Zoezi hilo limefanyika leo Januari 19, 2023 katika mtaa wa Mgodechi pembezoni kidogo ya mji wa Njombe kukutana na wakulima ambako pia kunapatikana moja ya duka la mfanyabiashara anayedawa kuuza mbolea feki,walisema kuwa mbolea hiyo ilikua na utofauti na mbolea nyingine ambazo wamewahi kutumia.

Ibrahimu kilunde mkulima wa viazi alisema mbolea hiyo ilikua tofauti na mbolea ambazo wamezoea kutumia kwenye msimu uliopita wa kilimo.

"Tulinunua ya kupandia na kukuzia madhara yake nimeyaona,mazao yananyauka kingine hata ardhi yenyewe itapata madhara kwa sababu tumetumia mara kwa mara,kuna mabadiliko ya rangi ina rangi zaidi ya tatu na ya zamani ilikua a rangi moja kama nyeupe ni nyeupe kama nyeusi inakua nyeusi"alisema

Zawadi Mgaya alisema kuwa mbolea hiyo inaujazo mdogo kuliko mbolea nyingine."Mimi nilinunu mifuko minne hadi sasa hivi ninayo nyumbani,ujazo ni mdogo sana ukilinganisha na mifuko mingine ambayo tuliwahi kununua sehemu nyingine"alisema Mgaya.

Kwa upande Adelina Stewele alisema alivyofika dukani aliomba kuuziwa mbolea aina ya DAP mifuko miwili lakini alivyofika nyumbani alikuta iko tofauti.

"Nilivyofika nyumbani wakati nafungua nakuta sio DAP na mbolea yenyewe nimetembea nayo hii hapa"alisema.

Aliongeza kuwa"Hata ujazo haijajaa,mfuko kawaida unashinwa mshono mmoja sasa huu ulikua umeshonwa mara mbili ukiwa umepinda pinda"alisema.

Geresius Ng'ande alisema alinunua DAP mifuko miwili"Wakati naweka kwenye shamba nakuta yani hayeyuki nikauuliza hii safari hii ni mbolea aina gani mbona ni vumbi nikafungua mwengine nao nikakuta ni vumbi kwa hiyo nikashindwa nikakuta habari kwamba vijana wamebaini mbolea feki"alisema Ng'ande.

Exaud Mgina alisema alipokwenda kununua mbolea hiyo aligundua utofauti na alipokwenda kuuliza dukani aliambiwa asubiri atabadilishiwa.

Kufuatia mkutano huo wakulima waliokumbwa na kadhia ya kuuziwa mbolea bandia wakatakiwa kurudi majumbani kwao na kujitokeza na mifuko waliyonunua kwa mfanyabiashara huyo.

Hata hivyo kulifanyika upimaji wa mbolea hizo na afisa udhibiti ubora wa mbolea TFRA nyanda za juu kusini Chimile Mfugale alibaini majina ya mbolea kwenye vifungashio ni tofauti na mbolea iliyopo ndani ya mfuko huku mbolea nyingine ikiwa na mchanganyiko usioeleweka.

Aidha mkuu wa mkoa wa Njombe Antony Mtaka aliwataka wananchi wote ambao wameuziwa mbolea hizo kujiandikisha majina kwa ajili ya kufanyiwa fidia.

"Jana kwenye nyumba ya huyu mfanyabiashara tulikamata mifuko elfu 10,532 ambayo ilikua ni mifuko imetoka kiwandani ni mitupu lakini yameandikwa majina ya hizi mbolea maana take alikua anafanya kazi ya kupriiti hii mifuko anakuja anachakachua anaandika minjingu kumbe DAP anaandika DAP kumbe minjingu anakuja anauza kernye maduka yake kama zoezi lile lingefanikiwa maana angefanya uchakachuaji wa mbolea kama alivyokua anauza hapa dukani kwa mifuko ile angefanikiwa angepata shilingi milioni 737,240,000"alisema.

Hata hivyo mkuu wa mkoa alisisitiza kutafutwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya dola mfanyabiashara huyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA USAILI MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 AGOST, 23 July 17, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI TAREHE 11-11-2021 October 27, 2021
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • AFISA HABARI WA HALMASHAURI ASHIKI KIKAO KAZI DAR ES SALAAM

    March 30, 2023
  • WAZIRI NAPE AWAFUNZA MAAFISA HABARI

    March 30, 2023
  • WAZIRI MKUU AFUNGUA KIKAO KAZI

    March 27, 2023
  • WAZIRI MKUU AZINDUA JARIDA MAALUMU LA MAFANIKIO YA KIPINDI CHA MIAKA 2 YA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

    March 27, 2023
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.