• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

MBUNGE AWAASA MADIWANI KUJIANDAA NA MIRADI YA LIGANGA NA MCHUCHUMA

tarehe Iliyowekwa: July 31st, 2021

Mbunge wa Jimbo la Ludewa Wakili Msomi Mhe. Joseph Zacharius Kamonga amewaasa Waheshimiwa Madiwani Katika Jimbo lake Kujipanga kuipokea miradi mikubwa ya uchimbaji madini ya Makaa ya mawe Mchuchuma na ule wa Chuma Liganga. Akizungumza katika Mkutano cha Baraza la Madiwani. Mhe. Kamonga amesema kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu imedhamiria kuhakikisha miradi hiyo inaanza utekelezaji wake. Amesema kuwa Waheshimiwa Madiwani wahakikishe wanajipanga katika maeneo yao ikiwemo kuona fursa ambazo zinaweza kuwanufaisha wananchi katika maeneo yao wanayoyaongoza. Mheshimiwa Mbunge alitolea mfano, kuanza kuona uwezekano wa kuwaandaa Vijana angalau wawili kutoka maeneo kata wanazoziongoza kuwezeshwa mafunzo ya ujuzi mbalimbali ili itakapofika muda kusikosekane nguvu kazi katika maeneo ya mradi, hali itakayopelekea wawekezaji kutafuta nguvu kazi nje ya maeneo yao, hususani Wilaya ya Ludewa kwa ujumla. 

Mheshimiwa Joseph Kamonga (Mb) alitilia mkazo suala hilo kwa kusema kwamba ni lazima kuona namna ya kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, kukaa na Wawekezaji kusaidia vijana kupata kozi za ujuzi (fresher course) kama vile udereva kwa vijana kadhaa kutoka kila kata ili kuwa na uwiano wa kunufaika na miradi hii mikubwa Wilaya nzima. Aidha, alisemea pia suala la ujenzi wa Chuo cha VETA katika Kijiji cha Shaurimoyo ambako ndiko uliko mradi wa Chuma-Liganga. Mheshimiwa Mbunge alitumia wasaa huo pia kuwapongeza Waheshimiwa Madiwani wote, Mkurugenzi wa Wilaya na Wataalamu kwa kufanikiwa kukusanya mapato vizuri na kuvuka lengo, ambapo kwa mwaka 2020/2021 Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa imekusanya wastani wa asilimia 112 na hivyo kwa mara ya kwanza kabisa Halmashauri hiyo kukusanya na kuvuka lengo la makusanyo. Halikadhalika amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya kupitia Ofisi ya Biashara kushughulikia kwa haraka madai ya wananchi ya kupanda kwa bei ya mafuta ya kula, kwani kwa maoni yake msimu huu wa mavuno ya mazao mbalimbali ikiwemo Alizeti bei haikupaswa kuwa juu sana mpaka wananchi wawe na malalamiko, pia kuhakikisha wanawatafutia wananchi soko la uhakika la Mahindi kwani ndio zao kuu la biashara na chakula katika Jimbo la Ludewa na Wilaya nzima kwa ujumla.

HABARI PICHA.

Picha 1: Katibu Tawala wa Wilaya ya Ludewa Bi. Zaina Mfaume Mlawa akiwasilisha salam za Serikali Kuu kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya. Kushoto kwake ni Bi Gladness Mwano Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya na katibu wa Mkutano huo wa Baraza la Madiwani akifuatiwa na Mhe. Wise Charles Mgina Mwenyekiti wa Halmashauri. 

Picha 2: Baadhi ya Waheshimiwa madiwani wajumbe wa Mkutano wa Baraza, wakiwa katika Mkutano wa robo ya nne na ya mwisho wa mwaka wa fedha wa 2020/2021. Msatari wa mbele kutoka kushoto ni Mhe. Joachim Lukuwi (Iwela), Mhe. Edgar Bosco Mtitu (Lubonde), Mhe. Hamis Kayombo (Mlangali), Mhe. Daniel Thomas Mhagama (Masasi) na Mhe. Rainalda Pius Tweve (Lupingu-Viti Maalum)

Picha 3: Baadhi ya Wananchi wa Ludewa waliohudhuria Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.