• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA LUDEWA AKUTANA NA VIONGOZI WA DINI NA KISIASA KUJADILI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

tarehe Iliyowekwa: September 26th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Ndugu Sunday Deogratias, jana alifanya mkutano muhimu na viongozi wa dini pamoja na viongozi wa vyama vya siasa kujadili maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba mwaka huu.


Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Deogratias alisisitiza umuhimu wa viongozi wa dini na siasa kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani, uwazi, na haki. Alieleza kuwa mchango wa viongozi hao katika kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu ni wa msingi kwa maendeleo ya demokrasia na ustawi wa jamii katika wilaya ya Ludewa.


“NINAWAOMBA VIONGOZI WA DINI NA VYAMA VYA SIASA KUWAHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA MCHAKATO WA UCHAGUZI, KICHUKUE FOMU NA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA. UCHAGUZI HUU NI FURSA YA KUJENGA SERIKALI ZA KIUWAJIBIKAJI NA ZENYE KUZINGATIA MAENDELEO YA WANANCHI,” alisema Deogratias.


Pia, Ndugu Deogratias alieleza kuwa serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa njia ya haki, huku akisisitiza kuwa vyama vya siasa vina wajibu wa kuepuka vurugu na maneno ya uchochezi. Aliongeza kuwa ni muhimu kila mgombea na chama kuzingatia taratibu na kanuni zilizowekwa ili kulinda amani wakati wa uchaguzi.


Kwa upande wa viongozi wa dini, waliombwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha jamii zinaendelea kuwa na utulivu, hususan katika kipindi hiki cha kampeni na uchaguzi. “VIONGOZI WA DINI MNA NAFASI YA KIPEKEE KATIKA KUWAONGOZA WANANCHI KUSIMAMA KATIKA ZILIZO SAHIHI, KUWEKA MBELE AMANI NA MAENDELEO YA JAMII YETU,” aliongeza.


Mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka madhehebu mbalimbali pamoja na viongozi wa vyama vya siasa ambao walitoa michango yao kuhusu namna bora ya kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa unafanikiwa na kutoa viongozi watakaowajibika kwa wananchi.


Mwisho, Ndugu Deogratias aliwataka wananchi wa Ludewa kushiriki kwa wingi katika mchakato wa uchaguzi kwa kujiandikisha, kuchukua fomu za kugombea, na kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili sauti yao isikike na kuchangia maendeleo ya jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.