• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ludewa District Council
Ludewa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Samaki
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Huduma za UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Kazi za Mwenyekiti Ofisini
  • Miradi
    • Miradi Iliyo Kwenye Mpango
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Habari Picha

KIWANDA CHA IDOFI KUANZA KUZALISHA DAWA IFIKAPO JANUARI, 2024.

tarehe Iliyowekwa: October 27th, 2023

Na. Chrispin Kalinga - Ludewa

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ameitaka  Wizara ya Afya na Bohari ya Dawa (MSD) kuhakikisha ifikapo Januari 2024 kiwanda cha Dawa Idofi kilichopo Makambako mkoani Njombe upande wa dawa kiwe kimeanza kuzalisha licha ya kuzalisha gloves ili kuendelea kuleta tija kwa wananchi.


Mhe. Dkt. Mpango ametoa  agizo hilo Jana tarehe 26 Oktoba, 2023 Mkoani  Njombe mara baada ya kuweka jiwe la  msingi katika kiwanda cha kutengeneza mipira ya Mikono (Gloves) kinachosimamiwa na Bohari ya Dawa (MSD).


Alieleza kuwa, lengo la kiwanda hicho ni kuhakikisha wanaboresha Huduma kwa jamii na kuimarisha afya za wananchi kwa kuzalisha upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi hapa nchini.


Dkt. Mpango alisema kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Uongozi imara wa Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwezesha upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa kuipatia mtaji Bohari ya Dawa ili kujenga viwanda zaidi vya dawa, maghala na kuongeza upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi nchini.


“Serikali inatambua vita iliyopo katika ujenzi wa viwanda vya dawa lakini kwa kuwa uamuzi huo ni wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hakuna atakayefanikiwa kuvikwamisha hivyo vitajengwa kwa manufaa ya taifa"


“Kwa sasa  serikali inaagiza dawa kwa asilmia 80 na vifaa tiba kwa asilimia 90 kutoka nje ya nchi, hali inayosababisha uhaba wa vifaa na gharama kubwa za uagizaji wa vifaa vya afya, ni lazima kuchukua maamuzi magumu ili kuweza kujitengemea katika upatikanaji wa dawa nchini”. Alisema Dkt. Mpango.


Aidha alisema kuwa, Rais  Samia ameamua viwanda vya dawa vijengwa kwa gharama yeyote kwa kuwa nchi ina uhaba  wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara.


“Tumeamua kuipatia MSD majukumu manne ambayo ni uzalishaji, ununuzi, utunzaji na usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi nchini hivyo ni niwahakikishie viwanda hivi vitajengwa nchini kwa maslahi ya taifa letu”, alisema Dkt. Mpango.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 10, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III, NA WITO WA USAILI WA ANA KWA ANA KWA WALIOCHAGULIWA November 11, 2021
  • TAADHARI YA UGONJWA WA POLIO LUDEWA March 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA KATIBU MAHSUSI III NA DEREVA II May 25, 2022
  • Tazama zote

Habari za Punde

  • MKUU WA WILAYA LUDEWA AUNGANA NA WANANCHI KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA MAZINGIRA

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI LUDEWA NA KUTEMBELEA MIRADI MITANO(5)

    May 07, 2025
  • WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MH. SELEMANI JAFO AAHIDI KUANZISHWA KWA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA HIVI KARIBUNI

    February 19, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, MHE. DKT. SELEMANI JAFO MKOANI NJOMBE, WILAYANI LUDEWA.

    February 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Dira na Dhima
  • Utawala na Rasilimali Watu
  • Historia
  • Misingi Mikuu
  • Orodha ya Madiwani
  • Miradi Iliyokamilika

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Tovuti Kuu ya Wananchi
  • Wizara ya Afya
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  • TANePS

Wanaotembelea Tovuti

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ludewa - Njombe

    Sanduku la Barua: 19

    Simu: 026-2790120

    Simu ya Rununu:

    Barua Pepe: ded@ludewadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2022Ludewadc . All rights reserved.